KWA NINI HAUPATI KILE UNACHOKITAKA AU HAUWI YULE UNAYEMTAKA?
Kwako mpendwa rafiki; Miaka kumi iliyopita nilikuwa nataka kuwa mwandishi wa vitabu vya hamasa! Ndiyo! Vitabu vya kuhamasisha wengine kubadili namna ya kufikiri na kupiga hatua kwenye mafanikio na maisha yao. Basi, nikiwa shule ya sekondari nilikuwa nikiandika makala mbali mbali za kuelimisha na kutoa hamasa kwa wengine. Kwa ufupi, nilikuwa najua nataka nini. Nataka kuwa nani. Lakini bado sikuweza kuwa mwandishi wa vitabu. Sikuwa najua namna ya kuwa ninayemtaka na kupata ninachokitaka. Mhhh hebu subiri kwanza; kwani wewe unajua…