Mambo mawili ambayo mtu yeyote hatakiwi kukuzidi
Rafiki, kwenye maisha na mafanikio unaweza kuzidiwa na mtu yeyote. Wala hilo siyo kosa wala tatizo. Unaweza kuzidiwa kipato, elimu na hata maisha mazuri. Wala isiwe kosa au dhambi. Pamoja na kuzidiwa huko, kamwe usiruhu mtu yeyote akuzidi kwenye vitu hivi viwili. 1. Kujifunza na kuchukua. Rafiki kama huwa haujifunzi huwezi kupiga hatua yoyote ile kuelekea kwenye mafanikio unayoyataka. Lakini pia kama utaishia kujifunza tu na usichukue hatua, bado hutaweza kupiga hatua. Hakikisha unakuwa mtu wa kujifunza na kuchukua hatua….