Browsed by
Month: April 2022

Mambo mawili ya kuzingatia ili kumpenda mwenza wako

Mambo mawili ya kuzingatia ili kumpenda mwenza wako

Rafiki, kama ilivyo umuhimu wa maarifa kwenye mafanikio yoyote yale, ndivyo ilivyo pia kwenye mahusiano ya ndoa. Hivyo kukosa maarifa juu ya mwenza wako na ndoa kwa ujumla ni chanzo cha mahusiano kufa. Ujinga huwa ni hatari sana kwenye mahusiano. Migogoro na mivutano mingi kwenye mahusiano ya ndoa ni kwa sababu wengi huwa hawajuani wala kufahamiana. Huwa wanashindwa kuelewe kwamba mwanamke na mwanamume huwa wanafikiri na kuwaza tofauti, na pia huwa wanayaona na kuyatafsiri mazingira yanayoeazunguka kwa mitazamo tofauti.! Hali…

Read More Read More

Hizi ni dalili za mtu anayejichukia na kujikataa kwenye mahusiano

Hizi ni dalili za mtu anayejichukia na kujikataa kwenye mahusiano

Rafiki, kama kuna kitu kibaya kwenye maisha ya mahusiano ni kujichukia na kujikataa mwenyewe. Mtu anayejichukia na kujikataa hawezi kuishi na mtu yeyote kwenye mahusiano. Mara nyingi watu wanaojichukia na kujikataa ni wale ambao wanaishi kwa yale yaliyo pita. Watu hawa wanapaswa kujua kuwa kilichopita kimeshapita. Vile tulivyokuwa au yale yaliyokwisha kututokea hayajalishi tena. Kinachojalisha ni vile tulivyo au vile kilivyo sasa na tutakavyo kuwa au kitakavyokuwa hapo baadaye. Pale unapoishi kwenye makosa yaliyopita, majuto na lawama hupelekea kujishusha hadhi,…

Read More Read More

Hili ni kosa kubwa unalofanya kwenye mahusiano yako.

Hili ni kosa kubwa unalofanya kwenye mahusiano yako.

Rafiki, kujichukia ni adui mkubwa sana kwenye mahusiano yako. Ni kosa kubwa ambalo watu hulifanya bila kujua madhara yake. Ukiwa unajichukia wewe mwenyewe, hutaweza kuishi kwenye mahusiano yoyote yale. Watu wengi hawawezi kuishi na watu wengine kwa sababu hawawezi kuishi wenyewe. Si hivyo hawawezi kutoa upendo wala kupokea kwa sababu wao wenyewe hawajipendi. Huwezi kutoa kile ambacho huna. Kama unajichukia wewe, huwezi kumpenda jirani yako kwa sababu unajichukia. Njia moja wapo ya kuwapenda wengine ni wewe kujipenda. Ni wewe kutokujichukia….

Read More Read More

Njia pekee ya kumjua na kumpenda mwenza wako

Njia pekee ya kumjua na kumpenda mwenza wako

Rafiki, hakuna kitu muhimu kwenye mahusiano ya ndoa kama kumjua mwenza wako. Unapaswa kumjua mwenza wako kuliko uavyoweza kumjua mtu yeyote duniani. Kumjua na kumfahamu mwenza wako ndiyo msingi na chanzo cha ndoa imara na yenye furaha. Ili uweze kumpenda mwenza wako unahitaji kumjua, kwani huwezi kumpenda usiyemjua. Siri ya ndoa yenye amani ni wanandoa kujuana kwa undani. Ukimjua mwenza wako, utakuwa huru. Ndiyo maana maandiko matakatifu yanasema, nanyi mtaifahamu kweli, na hiyo kweli itawaweka huru. Maana ya kuifahamu ni…

Read More Read More

Huu ndiyo upendo wa kweli unaopaswa kujenga mahusiano yako ya ndoa 4

Huu ndiyo upendo wa kweli unaopaswa kujenga mahusiano yako ya ndoa 4

Rafiki, mahusiano ya ndoa yanahitaji upendo wa kweli ili yaweze kuwa imara na ya kudumu. Pamoja na ukweli huo, upendo wa kweli umekuwa ni changamoto sana kwenye jamii yetu ya sasa. Watu wanaingia kwenye ndoa bila kuwa na uelewa wa ni upi upendo wa kweli na upi siyo upendo wa kweli. Watu wengi huchanganya kati ya aina nne za upendo, yaani upendo wa kirafiki ( Phileo love), Upendo wa kifamilia au kindungu (Storge love), Upendo wa kimapenzi au huba (Sexual…

Read More Read More

Huu ndiyo upendo wa kweli unaopaswa kujenga mahusiano yako ya ndoa 3

Huu ndiyo upendo wa kweli unaopaswa kujenga mahusiano yako ya ndoa 3

Rafiki, watu wengi hawaujui upendo wa kweli, licha ya kuwa wanausikia tu. Upendo wa kweli ni msingi mzuri wa kujenga mahusiano ya ndoa yaliyo imara na bora. Kutokuujua huku kunatokana na ukweli kwamba upendo wa kweli huchanganywa na aina nyingine za upendo; ambazo tunajifunza hapa ili kuweza kujua upi ni upendo wa kweli na upi siyo. Kama ulipitwa na makala juu ya aina za upendo tulizojifunza zisome hapa na hapa. Leo tunaendelea na aina nyingine ya upendo. Lengo ni kujifunza…

Read More Read More

Huu ndiyo upendo unaotakiwa kujenga mahusiano yako ya ndoa 2

Huu ndiyo upendo unaotakiwa kujenga mahusiano yako ya ndoa 2

Rafiki, ili kujenga mahusiano bora na ya kudumu unahitaji upendo. Upendo ni kiungo bora sana kwenye kujenga uhusiano wa ndoa imara. Pamoja na ukweli huo, si kila aina upendo unaweza kujenga ndoa iliyoimara. Kuna aina nne za upendo kutokana na lugha ya Kigiriki. Upendo wa kirafiki ( Phileo love), Upendo wa kifamilia au kindungu (Storge love), Upendo wa kimapenzi au huba (Sexual love) pamoja na Upendo wa kiMungu (Agape love). Lengo la kuzipitia na kujifunza aina hizi ni kujua upi…

Read More Read More

Huu ndiyo upendo unaotakiwa kujenga mahusiano yako ya ndoa

Huu ndiyo upendo unaotakiwa kujenga mahusiano yako ya ndoa

Rafiki, Upendo huwa ni kiungo muhimu sana kwenye mahusiano yoyote yale. Pamoja na ukweli huo, bado huwa kuna aina mbali mbali za upendo ambazo bila kuzielewa uimara na mapungufu yake hutaweza kujenga mahusiano ya ndoa yaliyo bora na ya kudumu. Si kila upendo ni msingi unaoweza kuutumia kujenga ndoa yenyefuraha furaha na amani. Ni muhimu kufahamu kuwa lugha yetu ya Kiswahili, kama zilivyo lugha zingine ikiwemo Kingeleza ni kutumia neno moja tu yaani “Upendo” kwa Kiswahili au “Love” kwa Kingeleza…

Read More Read More

Ni wapi unajifunza upendo wa kweli?

Ni wapi unajifunza upendo wa kweli?

Rafiki, upendo ni neno ambalo inasemekana ndiyo linaongoza kwa kutumika sana katika jamii yetu kwa sasa. Siyo tu kwenye mitandao ya kijamii, redioni, kwenye luninga, magazetini, kwenye vitabu, kwenye midomoya watu bali hata kwenye nyimbo wanazotunga na kuimba utalisikia, utaliona na kulisoma. Watu wengi wamefanya makosa kwa jina la upendo, wameua kwa jina la upendo, wametapeli na kudhurumu kwa jina la upendo. Si hivyo tu, kuna wanaooana kwa jina la upendo, lakini pia kuna wanaoachana au kutalikiana kwa jina la…

Read More Read More

Sifa mbili zinazofanya urafiki uwe kiungo muhimu kwenye ndoa

Sifa mbili zinazofanya urafiki uwe kiungo muhimu kwenye ndoa

Rafiki, ndoa ni mahusiano muhimu na ya awali kabisa, kwani hutangulia aina nyingine za mahusiano. Pamoja na ukweli huo, urafiki huwa ni kichocheo muhimu sana kwenye mahusiano ya ndoa, ili iwe na furaha na amani. Mahusiano yoyote yanapaswa kuhusisha urafiki ili yaweze kuwa bora, yenye furaha na amani. Uchumba unatakiwa upitie hatua hii muhimu ya urafiki, ili wahusika waweze kujuana kwa undani. Ni muhimu kutambua kuwa; mahusiano ya ndoa yasipofuatiwa na mahusiano ya urafiki kati ya mke na mume, ndoa…

Read More Read More