Browsed by
Month: January 2023

Mambo muhimu ya kujifunza kutoka kwa Mandoga

Mambo muhimu ya kujifunza kutoka kwa Mandoga

Mpendwa rafiki, Sina uhakika kama unamfahamu au ulishawahi kumsikia lakini kuna vitu vyingi muhimu vya kujifunza kutoka kwake.Huyu si mwingine bali ni bondia aliyejizolea maarufu sana siku za hivi karibuni nchini Tanzania. Alianza kama utani wakambeza, wakamcheka na wengine kumdharau na kumdhihaki pengine kwa sababu ya umri wake kuwa mkubwa, au kutokuwa na hisitoria yoyote kwenye mchezo wa ngumi si mwingine bali ni Karim Mandonga. Kwasasa Mandonga anaushawishi mkubwa kwenye ndondi pengine kuliko bondia yeyote hapa Tanzania. Si Mwakinyo, Dulla…

Read More Read More

Je, uko tayari kubeba majukumu kwenye ndoa?

Je, uko tayari kubeba majukumu kwenye ndoa?

Kwako wewe mpendwa rafiki yangu. Usioe au kuolewa kwa sababu ndugu zako wamekushauri, usiolewe au kuoa kwa sababu umri umekwenda, usioe au kuolewa kawa sababu marafiki zako wameoa au kuolewa. Usioea au kuolewa kwa sababu ya kutafuta uraia, pesa, fursa na mambo yafananayo na hayo, bali oa au olewa kwa sababu ukotayari kubeba majukumu. Uko tayari kujitoa kuachilia badhi ya vitu unavyovipenda ili uweze kuishi na mwenza wako. Ndoa inahitaji utayari wako wa kubeba majukumu. Usiingie kwenye ndoa kwa sababu…

Read More Read More

Kama huwezi kuitawala hamu ya tendo la ndoa, usiingie kwenye ndoa

Kama huwezi kuitawala hamu ya tendo la ndoa, usiingie kwenye ndoa

Kwako rafiki yangu mpendwa. Huwa zipo hamu au njaa nyingi kwenye mahusiano ya ndoa. Kuna hamu ya chakula, maji, usingizi, n.k . Lakini moja ya hamu muhimu ambayo inahitaji kulishwa na kushibishwa ni tendo la ndoa. Tendo la ndoa ni hitaji linalopaswa kutimizwa au wanandoa kutimiziana na wote wanapaswa kuridhika. Pamoja na ukweli huo, lakini tendo la ndoa ni zaidi ya hitaji. Ni hamu, ni kiu, ni njaa inayopaswa kushibishwa.  Unahitaji kujua kuwa, hamu yoyote ile tunaweza kuishibisha au kuikata…

Read More Read More

Je unayajua makusudi ya tendo la ndoa kwenye mahusiano ya ndoa?

Je unayajua makusudi ya tendo la ndoa kwenye mahusiano ya ndoa?

Kwako mpendwa rafiki. Rafiki, unajua nini kuhusu tendo la ndoa? Mbali na kuzaliana, je yapi ni makusudi ya tendo la ndoa? Na je unafahamu kuwa, tendo la ndoa ndiyo ndoa yenyewe? Kulingana na umuhimu wa tendo la ndoa kwenye mahusiano ya ndoa, hapa kuna makusudi haswa ya tendo la ndoa kwenye mahusiano ya ndoa ambayo ni muhimu kuyafahamu. Kwanza, tendo la ndoa ni kwaajili ya mawasiliano. Siku zote mahusiano ni mawasiliano. Moja ya njia nzuri ya kuwasiliana ni kupitia tendo…

Read More Read More

Tendo la ndoa ni njia muhimu ya mawasiliano kwa wanandoa

Tendo la ndoa ni njia muhimu ya mawasiliano kwa wanandoa

Kwako mpendwa rafiki. Tendo la ndoa ndiyo ndoa yenyewe. Likitumika vizuri kama lilivyokusudiwa, ni njia nzuri na muhimu ya kuwasiliana kimwili, kihisia, kiroho na kisaikolojia kwa wanandoa. Tendo la ndoa linaleta muunganiko wenye umuhimu. Linatengeneza bondi na kuuwaunganisha wanandoa. Kama likifanyika kwa usahihi na ukamilifu mkubwa, huwa linatibu migogoro mingi na changamoto zinazoibuka kwenye ndoa. Sasa changamoto ni pale tendo la ndoa linapotumika kinyume na kusudi lake. Kama nyinyi siyo wanandoa, na mkafanya tendo la ndoa, bondi hiyo inabaki ikiwa…

Read More Read More

Je unafahamu wewe ni dhahabu?

Je unafahamu wewe ni dhahabu?

Kwako rafiki mpendwa. Unafahamu kwamba wewe ni dhahabu? Ndiyo! Wewe ni wa thamani kubwa sana. Ni vile tu hujajua thamani uliyo nayo. Dhahabu huchimbwa chini sana, lakini pia ili iwe na thamani zaidi huwa inapitishwa kwenye moto ili kusafishwa na kughara zaidi. Changamoto unazokuwa unapitia ni kwa sababu ya dhahabu uliyonayo inazidi kusafishwa, ili iwe na thamani kubwa zaidi. Hivyo, kwanza usijidharau na kujiona hauna thamani. Pili, kuwa adimu na usiyepatika kwa kila mtu. Rafiki, unajua kinachoifanya dhahabu iweze kuendelea…

Read More Read More

Usiiruke hatua hii kwenye uchumba

Usiiruke hatua hii kwenye uchumba

Kwako mpendwa rafiki, Uchumba ni hatua muhimu sana kuelekea kwenye ndoa. Hatua hii ndiyo pia hutoa mwelekeo wa jinsi mambo yatakavyokuwa kwenye ndoa. Ndoa huwa haimbadilishi mtu bali ndiyo humfunua mtu na tabia zake. Hivyo ni muhimu kuitumia hatua ya uchumba ili kumjua vizuri mwenza wako unayetarajia kuingia naye kwenye ndoa. Pamoja na ukweli huo, kuna hatua moja ambayo hutakiwi kabisa kuiruka wakati wa hatua ya uchumba. Hatua hiyo ni hatua ya Urafiki. Hii ni hatua muhimu sana mnapokuwa kwenye…

Read More Read More

Je wewe unajijua? unamjua mwenza wako vizuri?

Je wewe unajijua? unamjua mwenza wako vizuri?

“Mjue mwenza wako vizuri na ishi naye vizuri kwenye ndoa” Ulikuwa ni ushauri alionipa mzee Sahani, Mwalimu mstaafu baada ya kukutana naye na kutaka kujua kwa undani maisha yake ya mahusiano ya ndoa yalikuwa je. Lengo la kukutana naye ni kutaka kujua kutoka kwake, sababu zilizomfanya akaoa wake kumi na wawili kwa wakati tofauti tofauti katika maisha yake ya mahusiano ya ndoa. Alikuwa akioa mwanamke anakaa naye mwaka mmoja au miwili anaachana naye, yaani alikuwa hawezi kuishi pamoja na mwanamke…

Read More Read More

Usichokijua kuhusu ndoa

Usichokijua kuhusu ndoa

Kwako rafiki mpendwa uliyeko kwenye ndoa au yule unayetarajia kuingia kwenye ndoa. Moja ya changamoto kubwa kwenye mahusiano ya ndoa ni kwa wanandoa au wale wanaotarajia kuingia kwenye ndoa ni kutokufahamu ndoa kwao inamaana gani. Hali hii hupelekea makosa na kufanyiana visa, vitimbi na kila aina ya visa kwa wanandoa. Ni muhimu kufahamu kuwa, ndoa ni chombo cha kuwafikisha kule mnakotaka kwenda. Ni kama boti inayotakiwa kuwavusha baharini. Huwezi kuingia kwenye boti kisha ukaanza kuitoboa, huku ukitegemea utavuka salama. Lazima…

Read More Read More

Wapenzi kujeruhiana ni wivu wa kimapenzi kweli?

Wapenzi kujeruhiana ni wivu wa kimapenzi kweli?

Rafiki, mahusiano ya ndoa huwa yanapita katika vipindi tofauti tofauti. Hakuna mahusiano yaliyonyooka. Kunakutofautiana kimtazamo, kiitikadi na hata kidini, lakini pamoja na kutofautiana huko maisha lazima yaendelee na umoja unahitajika. Wapo wanandoa au wapenzi ambao hawawezi kabisa kutatua changamoto na tofauti zao wanazokuwa wanapitia. Matokeo yake huwa ni kujeruhiana, kupigana na hata kupelekea wengi kuumizana na kuuana. Mara nyingi kile watu wanachoita ni wivu wa kimapenzi huwa siyo kwani hisia ya wivu huwa inalengo zuri la kukilinda na kukithamini kile…

Read More Read More