Browsed by
Month: November 2022

Siri ya mafanikio ni kufanya kile usichojisikia kufanya

Siri ya mafanikio ni kufanya kile usichojisikia kufanya

Kwako rafiki mpendwa, Nafahamu kwamba wewe huwa unafanya kile unachokuwa unajisikia kufanya; ndiyo maana uko hapo ulipo leo. Biashara zako haziendi, kazi zako haziendi, mahusiano yako yamekwama na maisha yako siyo mazuri. Unafanya kazi kwa bidii, juhudi na maarifa lakini bado mambo ni magumu. Habari njema ni kwamba leo na kwenda kukushirikisha siri moja muhimu ambayo itabadili kabisa biashara yako, kazi yako, mahusiano yako na maisha yako kwa ujumla. Ni siri ambayo hakuna serikali, ndugu, jamaa na rafiki aliyetayari kukwambia….

Read More Read More

Fanya kazi zaidi ya saa 40 kwa wiki au uwe na maisha magumu

Fanya kazi zaidi ya saa 40 kwa wiki au uwe na maisha magumu

Kwako mpendwa rafiki, Sina uhakika kama unajua au haujui lakini ni muhimu kuwambia hili. Kama unafanya kazi saa 40 kwa wiki unaishi maisha ya kawaida na magumu. Unamaisha ya kawaida na magumu kwa sababu kuna kanuni unakuwa unaivunja kwa kujua au kwa kutokujua. Ni bahati mbaya sana hakuna rafiki, ndugu, serikali au mjomba atakaye kuambia ukweli huu. Haya; tufanye kwamba hauijui: Kanuni hiyo inasema, fanya kazi zaidi ya saa 40 kwa wiki. Ndiyo! Kwa mtu wa kawaida, anayeishi maisha magumu…

Read More Read More

Wewe fanya kazi tu

Wewe fanya kazi tu

Kwako rafiki mpendwa, “Kaka mimi ni kijana wa umri wa miak 25 nimemaliza kidato cha 4 Kilombero sec kwa bahati mbaya nikafeli, nipo mtaani huu mwaka wa 6 sasa lakini hakuna ninachofanya kaka. Nimesoma kitabu chako jana tena hapa Chalinze lakini mimi mtoto wa Ifakara hapo V/60 hospital ya Cancer nikaona nikutafute bro labda nitapata msaada wowote toka kwako hata wa ushauri tu kaka” Huu ni ujumbe niliopokea kwenye simu yangu wiki iliyopita, siku ya Jumapili nikiwa nimepumzika. Baada ya…

Read More Read More

Kwa nini juhudi inalipa mara mbili kuliko kipaji?

Kwa nini juhudi inalipa mara mbili kuliko kipaji?

Kwako mpendwa rafiki, Nimekuwa nikiulizwa mara kwa mara swali hili juu ya kipaji na juhudi. Je, kati ya kipaji na juhudi kipi kinalipa zaidi? Najua na wewe pengine umekuwa ukijiuliza swali kama hilo au linalofanana na hilo. Leo na kwenda kulitolea majibu na ufafanuzi hapa. Iko hivi rafiki yangu; kipaji ni kipawa ambacho mtu anazaliwa nacho ili kimuwezeshe kutimiza kusudi lake hapa duniani. Kila kusudi ulilonalo huwalinaambatana na kipaji cha kukusaidia kulitimiza kusudi hilo. Hivyo ili kujua unakipaji gani, lazima…

Read More Read More

Huyu ndiye rafiki wa kweli

Huyu ndiye rafiki wa kweli

Mpendwa rafiki, kila mtu anaweza kuwa na marafiki wengi na wa aina mbali mbali kadili awezavyo yeye. Unaweza kuwa na marafiki kazini, chuoni, shuleni na hata pale unapoishi. Lakini ukweli ni kwamba, ukibadili kazi au eneo ulilopo sasa hivi utapoteza marafiki wengi. Kama ukipanda daraja/cheo leo, marafiki wengi watakuacha au utawaacha kutokana na wewe kuuanda cheo. Utakuwa na marafiki wapya kwenye hicho cheo au nafasi uliyohamia. Hivyo marafiki wengi ulionao kwa sasa wanatokana na nafasi uliyonayo na mazingira uliyopo kwa…

Read More Read More

Huwezi kufanya usichokijua

Huwezi kufanya usichokijua

Rafiki, ulishawahi kujiuliza kwanini huwa haufanyi kile unachopaswa kufanya? Kwani nini unaendelea kufanya yale unayofanya hata kama hayakuletei matokeo? Iko hivi rafiki yangu; huwezi kufanya usichokijua. Chochote unachokifanya kwa sasa ni kwa sababu unakijua. Na vile vyote ambavyo huvifanyi na ulipaswa uwe unavifanya lakini huvifanyi ni kwa sababu tu huvijui. Mfano, kumekuwepo na changamoto nyingi kwenye biashara na kazi siku hizi ambazo hupelekea biashara nyingi kufa. Moja ya changamoto hiyo ni wafanyakazi wengi kutokujua wanatakiwa kufanya nini kwenye biashara au…

Read More Read More

Amua kuumia badala kumia na kisha ndipo uamue

Amua kuumia badala kumia na kisha ndipo uamue

Rafiki, kwenye mafanikio, mahusiano na maisha kwa ujumla huwa kuna mambo mawili lazima yatokee, pale unapotaka kufanya maamuzi na kuchukua hatua. Mambo haya ni amua-umia, au umia-amua. Usisubiri mpaka uumie ndipo uamue kufanya kile unachopaswa kufanya, bali amua sasa na kisha pata maumivu. Faida ya kuamua sasa ni kwamba utaweza kuamua pia ni maumivu kiasi gani upate. Ni gharama ipi unayoilipa. Kumbuka, kila kitu huwa kina gharama unayopaswa kuilipa. Ni wewe tu kuamua kuilipa na kupiga hatua kwenye maisha yako….

Read More Read More

Kitabu cha Unaweza kuwa unayemtaka kitakuwa TBC1 leo.

Kitabu cha Unaweza kuwa unayemtaka kitakuwa TBC1 leo.

Rafiki, sina uhakikaki kama unataarifa hii, lakini ni muhimu wewe kufahamu. Leo kitabu cha Unaweza kuwa unayemtaka kitakuwa “live” yaani mbashara kwenye kipindi cha KURASA DARASA, cha TBC1. Muda ni saa kumi na nusu jioni. Kama unavyo jua, furaha ya mwandishi ni kuona kazi yake inasomwa na watu wengi, na kuwasaidi kutoka kwenye changamoto wanazopitia. Na wewe unaweza kusoma kitabu hiki na kutoka kwenye changamoto unayopitia.  Leo nakupa OFA ya kupata kitabu cha UNAWEZA KUWA UNAYEMTAKA kwa elfu 10 tu…

Read More Read More

Kuwa makini na kile unachokifanya

Kuwa makini na kile unachokifanya

Rafiki, je unajua kuwa kila unapofanya kitu kipya kwa mara ya kwanza, unatengeneza na uwezo? Kisha huo uwezo uliotengenezwa huzalisha hitaji ambalo lazima litimizwe. Nadhani bado hujanielewa, nasema hivi; kila unapofanya jambo lolote jipya kwa mara ya kwanza, huwa kuna uwezo unazalishwa na mwili wako ambao uwezo huo pia huzalisha hitaji linalotakiwa kutimizwa. Mfano; ukitumia madawa ya kulevya leo; najua wewe siyo mtumiaji lakini ni mfano tu. Kuna uwezo (capacity), unazalishwa ili kufanikisha madawa hayo na huwa huishii hapo tu…

Read More Read More